Posts

Showing posts from January, 2024

WAZUNGUMZAJI WA LUGHA ISIYOFUNGAMANA NA TAIFA LOLOTE DUNIANI KUKUTANA ARUSHA

Image
Mkutano  wa kimataifa wa watu wanaodaiwa kuzungumza Lugha inayoitwa   Esperanto wanatarajiwa kukutana Arusha katika mkutano wao unaotarajiwa kufanyika mwezi Augost   mwaka   huu 2024 Mkurugenzi wa kituo cha kimataoifa cha mikutano cha Arusha Bw Epraim Mafuru amesema watu zaidi ya 1.000 kutoka  mataifa   zaidi   ya 100   wanaozungumza lugha isiyo na asiyoufungamana   na Taifa   lolote Duniani   wanatarajiwa kukutana   Arusha kujadili namna lugha hiyo   inavyoweza kuyaunganisha mataifa yote Duniani .  Mmoja wa   wanachama wa Lugha hiyo   iliyopewa   jina la   Lugha ya ESPERANTO Bw Francis Gendo amesema hii ni mara ya kwanza   kwa wadau   wa Luga   hiyo   ambayo   kwa   sasa inazungumzwa na watu zaidi ya milioni tano kote Duniani kukutana katika nchi ya Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla Tayari Kamati ya maandalizi ya mkutano huo imeshakamilisha hatua za awali za ...

WANANCHI WANAOISHI JIRANI NA HIFADHI WATOBOA SIRI NZITO YA KUSHAMIRI KWA MIGOGORO KATI YAO NA WATENDAJI WA HIFADHI

Image
  Hivi karibuni mgogoro  wa  muda mrefu kati ya  wananchi  wa Kijiji cha Bugeri kilichoko wilayani  Karatu mkoani  Arusha na Hifadhi ya Taifa  ya  Ziwa  Manyara ulipata ufumbuzi baada ya serikali kuamua kumega eneo la ukubwa wa hekari nane (8) na kuligawa kwa wananchi waliokuwa wamelivamia , Taarifa ya uamuzi huo ilitolewa na mkuu  wa mkoa  wa Arusha Bw  John Mongela katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijjini hapo ambapo pia alitumia nafasi hiyo  kutoa  msimamo wa serikali. Kikao hicho pia kiliwashirikisha watendaji wa hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara akiwemo mkuu wa hifadhi hiyo Kamishna wa Uhifadhi Eva Malya ambaye alielezea mchakato waliopitia hadi kufikia hatua. pia  walikuwepo wataalam wa ardhi mkoa  wa Arusha walioongozwa na Mpima wa mkoa  Bw Dany Mruma ambaye alitoa  ufafanuzi wa kitaalam juu ya masuala ya mipaka na sheria zinazotumika. baada ya maamuzi hayo wananchi nao wakapata naf...

WATAFITI NA WAHADHIRI WA VYUO NCHI ZA SADC WAVUNJA UKIMYA,UTUPAJI OVYO WA TAKA

Image
  WATAFITI na wahadhiri  wa vyuo vikuu kutoka nchi  4 (nne) kati ya (kumi na sita )16 za SADC wamekutana jijini  Arusha kujadili namna ya kukabiliana na athari  za utupaji ovyo wa taka katika mimea na viumbehai wakiwemo wanyamapori kuptia mradi unaotekelezwa  na SADC kwa  kushirikiana na  wadau  mbalimbali ikiwemo  Jumuiya ya  Ulaya . Mwakilishi  wa  Sekretarieti  ya  SADC  anayesimamia  Rasilimali Dr. Geoge  Wambura amesema mradi  huo unatarajiwa  kuwa na tija  kubwa kwani  miongoni mwa  wadau wanaoutekeleza ni  wataalam waliobobea  kwenye  sekta ya utafiti wakiwemo  wahadhiri wa  vyuo  vikuu Miongoni  mwa  vyuo  vinavyoshiriki katika utekelezaji  wa  mradi  huo ni pamoja na chuo  cha utafiti na  usimamizi wa wanyamapri  Afrika  cha  Mweka , ambapo   mkuu  wa chuo  hich...