WAZUNGUMZAJI WA LUGHA ISIYOFUNGAMANA NA TAIFA LOLOTE DUNIANI KUKUTANA ARUSHA


Mkutano  wa kimataifa wa watu wanaodaiwa kuzungumza Lugha inayoitwa  Esperanto wanatarajiwa kukutana Arusha katika mkutano wao unaotarajiwa kufanyika mwezi Augost  mwaka  huu 2024

Mkurugenzi wa kituo cha kimataoifa cha mikutano cha Arusha Bw Epraim Mafuru amesema watu zaidi ya 1.000 kutoka  mataifa  zaidi  ya 100  wanaozungumza lugha isiyo na asiyoufungamana  na Taifa  lolote Duniani  wanatarajiwa kukutana  Arusha kujadili namna lugha hiyo  inavyoweza kuyaunganisha mataifa yote Duniani . 


Mmoja wa  wanachama wa Lugha hiyo  iliyopewa  jina la  Lugha ya ESPERANTO Bw Francis Gendo amesema hii ni mara ya kwanza  kwa wadau  wa Luga  hiyo  ambayo  kwa  sasa inazungumzwa na watu zaidi ya milioni tano kote Duniani kukutana katika nchi ya Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla



Tayari Kamati ya maandalizi ya mkutano huo imeshakamilisha hatua za awali za  kuwezesha wazungumzaji wa lugha hiyo  kukutana ikiwa ni Pamoja na kukamilisha taraatibu zote za kiserikali  kitaifa na kimataifa zinazohitajika.

Kwa mujibu wa wadau hao, Esperanto ni Lugha ambayo haina asili na taifa lolote duniani, na haifungamani na Lugha yeyote Duniani hivyo mtu yeyote anaweza kujifunza na kuitumia na wanasema imeanza kupata wafuasi wengi wakiwemo wasio na lugha za  asili

 Kwa habari  zaidi kuhusu lugha hii tembelea  AMTV uweze kuzipata kwa undani


Comments

Popular posts from this blog

TAMKO LA KULAANI MAUAJI......CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT)CHALAANI MAUAJI YA KIKATILI YA MTOTO MKOANI KAGERA

VIONGOZI CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT) WAPAZA SAUTI JUU YA HATUA ANAZOCHUKUA RAIS DR SAMIA

TAMWA-ZANZIBAR YATOA RAI WAKATI WA UANDAAJI SERA, SHERIA