UTUNZAJI WA MAZINGIRA WAANZA KULETA TIJA WILAYANI LONGIGO KUPITIA BIASHARA YA HEWA UKAA
Wananchi wa vijiji 16 vya wilaya ya Longido mkoani Arusha wamesaini makubaliano ya kuanza kunufaika na hewa ukaa kati yao na wawekezaji wa kampuni Soil for the Future Tanzania yanayoashiria wananchi hao kuanza kunufaika na hewa ukaa baada ya kuhifadhi mazingira ambayo yameanza kuwavutia wawekezaji hao wa rasilimali hiyo .
Wakizungumzia
hatua hiyo viongozi na watendaji wa
vijiji hivyo wamesema tayari wameshaingia
makubaliano ya awali ya miaka mitano na wawekezaji
hao mbapo kila kijiji
kitapata asilimia 51
ya mapato yatokanayo na hewa ukaa
kila mwaka.
Hata
hivyo wananchi hao akiwemo
Bw Simion Olotosoi amewataka wawekezaji hao kuheshimu makubaliano kwani
uzoefu unaonyesha kwamba licha ya kuwepo kwa mikataba mingi ya uwekezaji
asilimia kubwa haiwanufaishi wananchi kama
wanavyotarajia.
Kwa
upande wake mwakilishi wa mwekezaji kutoka kampuni hiyo ya Soil for the Future Tanzania Bw .Iddi Mfunda amewaondoa wananchi hao hofu hiyo
kwa kusema kuwa wakati wa utekelezaji wa mkataba huo kampuni
itaendelea kutoa elimu kwa
wananchi ya namna bora ya kuendelea kutunza
nyana za malishao
kwa kuendesha ufugaji unalinda mazingira
Katika
kuwahakikishia wananchi
hao kuwa mkataba huo utatekelezwa
Makubaliano ya wananchi na
mwekezaji huyo yameshudiwa
na mkuu wa
wilaya ya Longido
Bw Marco Ngumbi ambaye pia ameendelea kuwaondoa wananchi hao hofu juu
ya mradi huo
Aidha Bw Ngumbi amewataka wananchi wa vijiji vingine kuongeza juhudi ya kutunza mazingira ili kunufaika na fursa hiyo ambayo pia itaongeza malisho ya mifugo.
KWA HABARI ZAIDI FUATILIA AMTV ,UZIPATE KWA KINA .
Comments
Post a Comment