MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA TRA MKOA WA ARUSHA YATOA TUZO KWA WALIPAKODI, YAOMBA USHIRIKIANO ZAIDI

 


Watendaji  wa  Mamlaka ya mapato nchini TRA mkoa  wa  Arusha wametoa Tuzo kwa  baadhi  ya  walipakodi katika hafla iliyofanyika  Mount Meru hoteli huku  wakielezea mafanikio na baadhi ya changamoto zinazoendelea  kujitokeza katika ukusanyaji  wa Kodi ikiwemo biashara ya magendo 

Wakiwa katika hafla hiyo mkurugenzi  wa rasilimaliwatu  na utawala wa wa malaka  hiyo Bw Moshi  Kabengwe alisema pamoja na kazi kubwa ya kukusanya kodi inayofanywa na watendaji wa  mamlaka hiyo bado kuna tatizo kubwa la biashara ya magendo hasa katika maeneo ya mipakani .

Kutokana na hali  hiyo Kabengwe  amewaomba wananchi  wa mikoa ya pembezoni ukiwemo  wa Arusha  kuunga mkono jitihada za kudhibiti biashara za magendo  zinazofanywa na baadhi ya watu  maeneo ya mipakani  na  watu  wanaingiza na  kutorosha  bidhaa  bila  kulipa kodi .

 Hata hivyo mkurugenzi  huyo  aliwapongeza wafanyabiashara  na wadau wengine wanaoendelea  kushirikiana na TRA katika ukusanyaji wa kodi ambao baadhi yao  ndio  hao  wamepewa tuzo  kama ishara  ya kutambua mchango  wao.




 Kwa  wake meneja wa tRA mkoa  wa Arusha Bi Eve Rafael amesema Pamoja na changamoto zilizopo  pia kuna  mafanikio  makubwa na Pamoja na kuwepo  kwa  baadhi ya  wanaoendelea kukiuka sheria asilimia  kubwa  wanaendelea kulipakodi kwa hiyari na  kutoa ushirikiano  katika ulipaji  wa  kodi  na  ameahidi  kuendelea  kuwapa  ushirikiano .



Mgeni rasmi   katika hafla hiyo  alikuwa  ni  mkuu  wa wilaya  ya  Arusha  Bw Felician Mutahengerwa  amewapongeza  watendaji wa TRA kwa  kujenga mahusiano mazuri  na walipakodi  na  kupata  mafanikio  makubwa  utaratibu  ambao  unafaa kuogwa  na  taasisi  na  idara  zingine  zikiwemo  halmashauri..bw felisian mtahengerwa  .

 kwa mujibu wa watendaji wa TRA pamoja  na changamoto  zilizopo  ushirikishaji  na  ushirikiano  wanaopata  kutoka  kwa wananchi  umewezesha  kufikia  na  kuvuka  malengo  ya ukusanyaji  wa  kodi .

kwa undani  zaidi  wa  habari  hii  tembelea  AMTV...UPATE HABARI KWA  KINA 

Mwisho  .

Comments

Popular posts from this blog

TAMKO LA KULAANI MAUAJI......CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT)CHALAANI MAUAJI YA KIKATILI YA MTOTO MKOANI KAGERA

VIONGOZI CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT) WAPAZA SAUTI JUU YA HATUA ANAZOCHUKUA RAIS DR SAMIA

TAMWA-ZANZIBAR YATOA RAI WAKATI WA UANDAAJI SERA, SHERIA