TAMKO LA KULAANI MAUAJI......CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT)CHALAANI MAUAJI YA KIKATILI YA MTOTO MKOANI KAGERA


 

TAMKO LA (CCWWT) KULAANI  MAUAJI  YA KIKATILI  YA  MTOTO  ASIMWE . 

Chama cha wazee  wanaume Tanzaniaa  (CCWWT)kimeungana  na  Rais Mh Dr Samia Suluhu Hassan na wadau  wengine  kulaani kitendo cha kuuawa kikatili  kwa Mtoto  Asimwe  Novati  mwenye ulemavu wa Ngozi (Albino) akiwa na umri wa miaka miwili na nusu yaliyotokea kijiji cha Gulamula Wilaya ya Muleba Mkoa wa Kagera

Akitoa tamko hilo  kwa niaba ya chama  kiongozi mkuu  wa chama hicho Bw Tadey Mchena amesema wanachama  wa chama cha wazee  wanaume kimesikitishwa  sana na ukatili  huo aliofanyiwa mtoto huyo na kuendelea  kusisitiza umuhimu wa  hatua kalia  za  kisheria  kuchukuliwa kwa  waliohusika.

Aidha  kwa  mujibu wa Bw Mchena chama cha  wazee  wanaume Tanzania  kiko  tayari kutoa ushirikiano wa hali na mali katika  kukabili vitendo hivyo vya kikatili vinavyofanywa na baadhi ya watu ambavyo  kwa  ujumla havikubaliki kwa namna yeyote,na mahali popote Duniani na hata Mbinguni .

Sisi viongozi na wanachama wa CCWWT  tunaungana na Mh Rais Dr Samia Suluhu hasan na wasaidizi wake akiwemo makamu wa Rais Mh Dr Philip Mpango ,Waziri Mkuu Mh Kasim Majaliwa ,Naibu Waziri  Mkuu Mh Dr Dotto Biteko  na Waziri wa maenndeleo ya Jamii jinsia na makundi  maalum Mh Dorosi  Gwajima kutoa  pole kwa familia ndugu , na jamaa wa Marehemu Mtoto Asimwe  Novati.

Aidha tunaiomba Jamii yote  kwa  ujumla kutokubali vitendo kama hivi  kujitokeza katika maeneo yao na kuona umuhimu wa  kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola kuwadhibiti watu hawa  wachache wanafanya vitendo hivi .

Na pia chama  kinawaomba wazee  wote wanaume popote  walipo Tanzania bila kujali  itikadi zao na tofauti zao za aina yeyote ile waungana na Mh Rais Dr Samia  na wasaidizi wake katika kupambana na ukati huu kwani  ni jambo  linalowezekana.

Imetolewa  na  Idara ya  Habari  na mawasiliano Chama cha  wazee  wanaume Tanzania  (CCWWT).

Comments

Popular posts from this blog

WAZIR PEMBE ATAKA UZINGATIAJI AFYA YA AKILI

VIONGOZI CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT) WAPAZA SAUTI JUU YA HATUA ANAZOCHUKUA RAIS DR SAMIA