VIONGOZI CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT) WAPAZA SAUTI JUU YA HATUA ANAZOCHUKUA RAIS DR SAMIA

 


   





 Viongozi  wa  Chama cha wazee wanaume Tanzania kinachoitwa (CCWWT) chenye makao yake makuu Jijini  Arusha wametoa pongeza  kwa Rais Dr Samia Suluhu Hassan kwa hatua anazoendelea  kuchukua kwa watendaji  wa serikali  wanaokiuka sheria taratibu na maadili  ya  Uongozi

Miongoni mwa hatua zilizozungumziwa  na  viongozi wa  chama hichi  ni pamoja  na ya kutengua uteuzi  wa  Naibu waziri wa katiba  na  sheria Mh Paulina Gekulu kwa kutuhumiwa kushiriki katika vitendo vinavyodaiwa  kukiuka sheria  suala ambalo  wazee  wanasema  yeye kama  kiongozi anayesimamia sheria  hangepashwa  kulifanya 

Viongozi hao akiwemo mkuu wa CHAMA hicho Bw Tadei Mchena amesema Mh Rais Dr Samia Suluhu Hassan ameonyesha njia kwa vitendo ya uongozi unaosimamia utawala Bora .

"Kwa niaba ya chama Cha wazee Wanaume Tanzania CCWWT tunamshukuru sana MH,Rais Dr Samia Suluhu Hassan kwa hatua anazoendelea kuchukua dhidi ya viongozi wanaoshindwa kukinda maadili ya majukumu waliopewa ambao kimsingi licha ya kupiteza sifa ya kuwa viongozi wanaleta picha mbaya kwenye jamii.

Sisi kama wazee Wanaume Tanzania tunaunga mkono hatua hizi na tunamwambia Mh Rais aendeleze utararatibu huo kwani una tija KUBWA sana katika jamii na taifa kwa ujumla na pia tunamuahidi Mh Rais Dr Samia kwamba sisi chama Cha wazee Wanaume Tanzania tutamuunga mkono na tutatumia zetu na uwezo WETU kumsaidia .

Kwa Sasa tunajipanga kufanya ziara nchi nzima kutoa elimu kwa jamii Juu ya kusaidiana na serikali kupambana na vitendo vyote ukatili na ukiukwaji wa maadili vinavyoendelea kushika kasi na tumeshaanza hatua za awali za kutekeleza azma hiyo ikiwemo ya kukisanya nguvu.alisema  Mchena Kiongozi mkuu wa Chama cha wazee  wanaume Tanzania







Kiongozi mwingine aliyezungumzia hatua hiyo ni pamona na ni Bw Michael Mwamaja ambaye ni Mweka hazina wa Chama yeye  amesema anachokifanya Mh  Rais Dr Samia kwa Sasa ni moja na mambo ambayo watanzania wengi wameyasubiri kwa muda mfefu .

Bw Michael Mwamaji amesema kinachomgusa zaidi juu ya maamuzi ya Dr Samia Suluhu Hassan ni namna anavyojipambanua kutekeleza kwa vitendo sera ya utawala bora ambayo licha ya kuwa nzuri na yenye lengo la kuongeza uwajibikaji, kwa muda mrefu imekuwa wimbo ambao hauna utekelezaji kwa vitendo.

"Kwa kweli Mh, Rais Samia amenigusa sana anachokifanya huo ndio utawala bora na tunamuombea mungu, aendeleze na utararatibu huo kwani utaongeza uwajibikaji kwa wanaopewa majukumu na sisi chama cha wazee Wanaume Tanzania tunamuunga mkono na pia tungewaomba watanzania tumuunge mkono na tumpe ushirikiano.

Hilo suala la utawala bora ndilo ambalo tunalipigia kelele muda mrefu sana,kwamba mtu akifanya kosa awajibike  mwenyewe ama awajibishwe na sio kubadilishiwa nafasi  wakati kwa sasa Tanzania hatuna uhaba wa watendaji wala wataalam,hivyo hakuna sababu kabisa ya kuwakumbatia wasiotaka kuwajibika na hili likisimamiwa vizuri,ufanisi utaongezeka kwani kila mmoja,atakuwa makini.

Sisi tunamwambia Mh Rais akaze uzi kwani kila kitu kiko wazi,na kila mmoja anajua wajibu wake,wala asimuangalie mtu usoni,mtu yeyote anayekwenda kinyume na taratibu,awajibishwe kwa  manufaa ya nchi yetu."alisema Bw.Mwamaji.






Hatua ya Mh Dr.Rais Samia Suluhu Hassan ya kuonyesha kwa vitendo utekelezaji wa utawala bora pia ikazungumziwa na baadhi ya wastaafu wataalam  akiwemo Bw.Michael Kingazi ambaye ni mtaalam wa afya mstaafu, yeye pamoja na kuungana na wengine kuongeza Rais Dr Samia,ameshauri suala la uwajibikaji na kuwawajibisha wasiofuata maelekezo zifanyike  kwa wote  wanaofanya makosa yakiwemo ya kushindwa kusimamia taasisi na idara walizopewa  na kwamba kipimo Cha kiongozi kufanikiwa ama kutofanikiwa kiwe ni matokeo ya idara na taasisi wanazoziongoza.

"Hakuna kosa dogo yote ni makosa na tukifumbia macho makosa madogo ndio yanaozaa makosa makubwa,hata vitabu vya mungu vinasema hakuna dhambi ndogo na kubwa zote ni dhambi tu"alisema Kingazi.

Miongoni mwa majukumu makubwa ya chama Cha wazee Wanaume Tanzania (CCWWT) ni pamoja na kushirikiana na Wadau wengine ikiwemo Serikali kukemea vitendo vya ukatili vinavyoendelea kushika kasi katika jamii,kukabiliana na mmomonyoko wa maadili katika jamii sambamba na kutoa elimu ya athari zake.

MWISHO. 

 

Comments

Popular posts from this blog

TAMKO LA KULAANI MAUAJI......CHAMA CHA WAZEE WANAUME TANZANIA (CCWWT)CHALAANI MAUAJI YA KIKATILI YA MTOTO MKOANI KAGERA

TAMWA-ZANZIBAR YATOA RAI WAKATI WA UANDAAJI SERA, SHERIA