BENK YA CRDB YAENDELEA KUPASUA ANGA KIMATAIFA, SASA YABISHA HODI MAREKANI.
Benk
ya CRDB imeendelea kuwa kinara wa kujenga mtandao mkubwa wa huduma za
kifedha kitaifa na kimataifa
baada ya kuingia makubaliano ya ushirikiano katika utoaji
wa huduma na Benki ya kimataifa ya American Express ya nchini
Marekani.
Katika makubaliano hayo wateja wa Benk ya American
Expres na wale
wa Benk ya CRDB watakuwa na kadi
ambayo itaweza kutumika kwenye mashine za ATM za benk zote mbili popote Duniani .
Akizungumza
wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo Mkurugenzi
Mtendaji wa Benk ya CRDB Bw Abdul Majid Nsekela
amesema hatua hiyo itapunguza
gharama na pia mzigo wa kutembea na
fedha fursa ambayo itawanufaisha hasa wanapokuja kutalii nchini.
Kwa
upande wake mwakilishi wa Benk hiyo ambaye pia ni Makamu wa Rais wa American Express anayewakilisha
nchi za Ulaya, Mashariki ya Kati na pia Afrika Bi Briana Wilsey amesema kutokana na mtandao
mkubwa wa Benk hiyo kote duniani
usirikiano huo utakuwa na tija
kubwa katika nchi mbalimbali
ikiwemo Tanzania na ameipongeza Benk ya CRDB kwa kuwa miongoni mwa Benk zinazokua kwa kasi na zenya mtandao mkubwa kaika ukanda wa Afrika mashariki..
Akizungumza baada ya uzinduzi huo mkuu wa mkoa wa Arusha Bw.John Mongela amesema hayo ni
mafanikio makubwa na ni matokeo ya kazi kubwa inayofanywa na serikali ya Tanzania chini ya Mh,Rais Dr
Samia Suluhu Hassani ya
kuimarisha sekta ya utalii.
Watendaji wa Benk ya CRDB akiwemo makamu mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Benk hiyo Profesa Neema Mori amesema wanajivunia mafaniko makubwa ya Benk hiyo ambayo ni matokeo ya kazi nzuri na kubwa wanayoendelea kuifanya ya kuimarisha utoaji wa huduma.
Baadhi ya wadau wa utalii wameipongeza Benk ya CRDB kwa hatua iliyofikiaambapo kwa sasa inatoa huduma katika nchi mbalimbali za Afrika Mashariki ikiwemo Burundi na Kongo.
Kwa Habari
zaidi usikose kutembelea AMTV
upate habari kwa
kina.
Comments
Post a Comment