Posts

Showing posts from October, 2023

WANACHAMA WAMCHAGUA TENA MLAY KUWA RAIS MCT

Image
  NA HAJI NASSOR, ARUSHA WANACHAMA wa Baraza la Habari Tanzania MCT, wamemrejesha tena Rais wa Baraza hilo, Jaji Mstaafu: Juxon Isaac Mlay kwa miaka mengine mitatu ijayo, kupitia mkutano mkuu wa 25, uliofanyika Septemba 28, 2023 mkoani Arusha. Mkutano huo, pia umemchagua Yussauf Khamis Yussuf kuwa Makamu wa rais  na wingine waliochaguliwa katika mkutano huo ni wawakilishi wa vyombo vya habari, akiwemo Tido Mhando. Wawakilishi wingine ni Rose Rouben, Ali Haji Mwadini samba mba na kupatikana kwa wawakilishi watatu, kundi la umma wakiongozwa na CPA: Happiness Nkya, Jaji Robert Makaramba na Mwajaa Said. Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, rais aliyerejea tena madarakani Juxon Isaac Mlay, alisema kasi na ari iliyokuwepo kwa miaka mitatu, ni vyema ikaongezeka. Aliwataka viongozi wenzake, waliorudi kutetea nafasi zao, kuhakikisha wanaendelea kufanya makubwa, wakiwa ndani ya Baraza la Habari Tanzania, ili kuwalipa wanachama waliowachagua. ‘’Niwaombe wale viongo...

KAMANDA MCHOMVU AWAPA NENO WAZAZI

Image
KAMANDA   wa polisi Mkoa wa Mjini Magharibi kamishina Msaidizi wa  P olisi Richard  (ACP),  Thadei Mchomvu, amewataka wazazi na walezi  kushirikiana kwa pamoja katika kuwalea na kuwatunza watoto wao kwa ajili ya kuwalinda   na vitendo vya ukatili na udhalilishaji. Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili ofisini kwake Muembe Madema  M jini Zanzibar, amesema baadhi ya wazazi   hushughulikia  shughuli zao zaidi na hawana utamaduni wa  kuwa  karibu na watoto wao jambo  ambalo hupelekea kuendelea vitendo hivyo. "Wapo wazazi wakitoka  asub u h i ndo wametoka kurudi kwao ni usiku watoto wakiwa wamelala, mtindo ambao unachangia watoto kukosa elimu ya kujitambua  iliyo muhimu katika kuwasaidia kuepuka kufanyiwa vitendo viovu vya kudhalilishwa," a lisema Richard " Na baadhi ya kina mama wanawacha watoto kudhurura ovyo bila ya kuwavisha nguo kamili na kupelekea mtoto kufanyiwa vitendo...

MRADI WA ‘SWIL’ ZANZIBAR, ULIVYOWAONESHA NJIA WANAWAKE KUDAI HAKI ZAO: TAMWA, PEGAO ZASEMA JAMBO

Image
  NA HABIBA ZARALI, PEMBA  HAWAKUKOSEA waliosema 'umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu' Msemo huu umesadiki katika utekelezaji wa mradi wa kuwawezesha wanawake kudai haki zao za uongozi , demokrasia na siasa 'SWIL' unaotekelezwa kwa mashirikiano kati ya    TAMWA Zanzibar, ZAFELA na PEGAO. Mradi huo ambao ulizinduliwa mwaka 2020 na kutarajiwa kumalizika 2023 umeonekana na mafaniko makubwa katika hatuwa mbalimbali za utekelezaji wake. Utekelezaji wa mradi huo ambao ulitarajiwa kuwafikia na kuwawezesha wanawake 6000 kwa zanzibar, Unguja na Pemba katika kudai haki zao ili nao waweze kuwawezesha wengine tayari umeonyesha njia katika kufikia hatuwa ya kudai haki zao za uongozi.   Mradi huo wa SWIL ambao unafadhiliwa na ubalozi wa Norway umetekelezwa maeneo mbalimbali ambapo kwa upande wa    Pemba tayari      umeshawafikia wastani wa wanawake 4000.   Katika hatuwa za kufanikisha lengo la mradi la kuwawezesha wanawake kudai haki zao za uon...

TAMWA-ZANZIBAR YATOA RAI WAKATI WA UANDAAJI SERA, SHERIA

Image
  NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar Dk. Mzuri Issa  Ali ameishauri Serikali pamoja na Taasisi binafsi kuandaa Sera na Sheria za nchi kwa kuzingatia usawa na jinsia zote ili kuwepo usawa wakati wa teuzi mbali mbali zinazofanywa. Akizinduwa waraka maalumu naoainisha changamoto zinazowakumba wanawake na watu wenye ulemavu katika kugombea nafasi za Uongozi hafla iliyofanyika Ofisi za ukumbi wa bima Mperani mjini Unguja. Dk.Mzuri amesema kwa miaka mingi wanawake na watu wenye ulemavu wamekosa nafasi muhimu katika ngazi za maamuzi jambo ambalo linawanyima haki yao ya msingi ya kidemokrasia ya kutoa mawazo yao na uhuru wa kujieleza. “Elimu ndio ngazi kubwa ya kuwapeleka wanawake katika Uongozi kwa miaka mingi iliyopita walinyimwa fursa ya elimu na baadhi ya wazee ama walezi kutishwa na kuwa na dhana potofu ya kuharibiwa watoto wao katika masuala ya udhalilishaji na kwa bahati mbaya fursa hizo kupata wanaume pekee,”  a...

JAMII YAKUMBUSHWA KUILINDA HAKI KUU YA BINAADAMU

Image
  NA ASHA ABDALLA, PEMBA JAMII imekumbushwa kuwa, moja ya haki kuu ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni kosa kwa mtu mwengine yeyote kumuondolea mwenzake . Hayo yalielezwa na mtoa mada mwanasheria kutoka Shirika la Msaada na Haki za Binaadamu Siti Habib Mohamed, wakati akiendesha mafunzo ya siku nne kwa waandishi wa habari, wadau wa habari na wasaidizi wa sheria, yanayofanyika Chuo cha Amali Vitongoji Chake chake na kuandaliwa na Mwemvuli wa asasi za Kirai Pemba PACSO kwa ufadhili wa UNDP. Alisema kua zana ya haki za binadamu ilianzishwa mnamo  mwaka 1948 baada ya vita vya kwanza vya dunia, hivyo ni wajibu wa kila mmoja hadi leo hii, kuhakikisha anailinda na kuitetea haki ya kuishi ya mwanzake. Alieleza kuwa, haki za binadamu kimsingi ni yale madai au haki zote ambazo anadai binamu mara baada ya kuzaliwa, na kwa kawida hakuna taasisi yoyote ambayo inaweza kuzuia. ‘’Ni kweli haki ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuh...

DK. MZURI AONESHA UMUHIMU WA SHERIA BORA ZA HABARI

Image
  Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania (TAMWA ZNZ) Dkt. Mzuri Issa amesema ni muhimu kuwa na sheria bora za habari ambazo zinapelekea kuwepo kwa uhuru wa habari na uhuru wa kujieleza kwa jamii. Amesema hayo wakati wa mkutano wa kutoa mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya tume ya utangazaji ya Zanzibar (No. 7, 1997), ambao uliwashirikisha kamati ya masuala ya habari (ZAMECO), Asasi za kiraia na Tume ya kurekebisha ya Sheria uliofanyika  Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mazizini. Dkt.  Mzuri aliongeza  kuwa ipo haja ya kufanyiwa marekesbiso sheria hiyo ili kutoa fursa ya uhuru wa kujieleza ambao ndio chanzo kikuu cha maendeleo ya nchi. “ Uhuru wa habari na haki ya kupata habari pamoja na uhuru wa kujieleza ni mambo ya msingi katika maendeleo ya nchi na inaleta  furaha ya mtu binafsi”, amesisitiza Dkt. Mzuri Issa. Kwa upande wake,  Mwenyekiti wa tume ya kurekebisha sheria Zanzibar, Ndugu  Khadija Shamte amesema kuwa muda umef...

WAZIR PEMBE ATAKA UZINGATIAJI AFYA YA AKILI

Image
  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amewataka wananchi kuzingatia umuhimu wa Afya ya akili ili kuzuia maafa ambayo yanayoweza kutokea na kupelekea athari kubwa kwa katika mwili wa binadamu. Akizungumza katika  bonanza la kuadhimisha kuelekea siku ya afya ya akili na maafa duniani lilofanyika katika jengo la Chuo cha Afya Zanzibar Wilaya ya Magharib “B” Unguja, amesema   kila mwananchi anapaswa kutambua umuhimu wa afya ya akili kama ilivyo afya ya mwili ili kujikinga na maafaa ambayo yanawezakujitokeza. Amesema afya ya akili ni muhimu kwa kila mtu kwani inamuwezesha kuishi maisha yenye furaha, tija na kujisikia vizuri ulimwenguni. Lakini mara nyingi suala hili halipewi kipaumbele kinachostahili.  Hivyo Waziri huyo  amehimiza suala la afya ya akili kupewa kipaumbele na kila mtu, kutambua kwamba  ni sehemu muhimu ya afya kwa ujumla. “Afya ya Akili ni muhimu kwa kila mmoja wetu, kwani maafa hay...

Hizi hapa nchi zinazoongoza kwa kutokua na furaha.

Image
Denmark imechukua nafasi ya Switzerland kama nchi yenye furaha zaidi duniani kwa mujibu wa ripoti iliyotoka Jumatano hii. Ripoti hiyo imeandaliwa na ‘Sustainable Development Solutions Network and the Earth Institute’ katika chuo kikuu cha Columbia. Ilionesha kuwa Syria, Afghanistan na nchi zingine 8 zilizopo chini ya jangwa la Sahara ndizo sehemu zisizo na furaha zaidi. Nchi hizo ni pamoja na Madagascar, Tanzania, Liberia, Guinea, Rwanda, Benin, Togo na Burundi. Nchi 10 za juu zenye furaha zaidi ni Denmark, Switzerland, Iceland, Norway, Finland, Canada, Uholanzi, New Zealand, Australia na Sweden. Nchi tano duniani, Bhutan, Ecuador, Scotland, UAE na Venezuela zimeteua mawaziri watakaoshughulikia ukuzaji wa furaha. Tanzania tuna matatizo gani? Kuna umuhimu wa Magufuli kuanzisha wizara kama hiyo pia?